100 | GEN 4:20 | Ada akamzaa Yabali ambaye ni baba wa wale walioishi katika mahema na kufuga wanyama. |
101 | GEN 4:21 | Kaka yake aliitwa Yubali, aliyekuwa baba wa wote wapigao zeze na filimbi. |
121 | GEN 5:15 | Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi. |
122 | GEN 5:16 | Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike. |
124 | GEN 5:18 | Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki. |
125 | GEN 5:19 | Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike. |
126 | GEN 5:20 | Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa. |
135 | GEN 5:29 | Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.” |
138 | GEN 5:32 | Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi. |
148 | GEN 6:10 | Noa alikuwa na wana watatu: Shemu, Hamu na Yafethi. |
173 | GEN 7:13 | Siku hiyo Noa, na mkewe, na wanawe Shemu, Hamu na Yafethi pamoja na wake zao wakaingia katika ile safina. |
212 | GEN 9:6 | “Yeyote amwagaye damu ya mwanadamu, damu yake itamwagwa na mwanadamu, kwa kuwa katika mfano wa Mungu, Mungu alimuumba mwanadamu. |
224 | GEN 9:18 | Wana wa Noa waliotoka ndani ya safina ni: Shemu, Hamu na Yafethi. (Hamu ndiye alikuwa baba wa Kanaani.) |
229 | GEN 9:23 | Lakini Shemu na Yafethi wakachukua nguo wakaitanda mabegani mwao wote wawili, kisha wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zilielekea upande mwingine ili wasiuone uchi wa baba yao. |
233 | GEN 9:27 | Mungu na apanue mipaka ya Yafethi; Yafethi na aishi katika mahema ya Shemu, na Kanaani na awe mtumwa wake.” |
236 | GEN 10:1 | Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika. |
237 | GEN 10:2 | Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi. |
239 | GEN 10:4 | Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu. |
256 | GEN 10:21 | Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi. |
260 | GEN 10:25 | Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani. |
261 | GEN 10:26 | Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera, |
264 | GEN 10:29 | Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani. |
318 | GEN 12:19 | Kwa nini ulisema, ‘Yeye ni dada yangu,’ hata nikamchukua kuwa mke wangu? Sasa basi, mke wako huyu hapa. Mchukue uende zako!” |
329 | GEN 13:10 | Loti akatazama akaona lile bonde lote la Yordani kuwa lilikuwa na maji tele, kama bustani ya Bwana, kama nchi ya Misri, kuelekea Soari. (Hii ilikuwa kabla Bwana hajaharibu Sodoma na Gomora.) |
330 | GEN 13:11 | Hivyo Loti akajichagulia bonde lote la Yordani, akaelekea upande wa mashariki. Watu hao wawili wakatengana: |
434 | GEN 18:9 | Wakamuuliza, “Yuko wapi Sara mkeo?” Akasema, “Yuko huko, ndani ya hema.” |
488 | GEN 19:30 | Loti na binti zake wawili waliondoka Soari na kufanya makao yao kule milimani, kwa maana aliogopa kukaa Soari. Yeye na binti zake wawili waliishi katika pango. |
562 | GEN 22:14 | Abrahamu akapaita mahali pale Yehova-Yire. Mpaka siku ya leo inasemekana, “Katika mlima wa Bwana itapatikana.” |
570 | GEN 22:22 | Kesedi, Hazo, Pildashi, Yidlafu na Bethueli.” |
597 | GEN 24:5 | Yule mtumishi akamuuliza, “Je, kama huyo mwanamke atakataa kuja nami katika nchi hii? Je, nimpeleke mwanao katika hiyo nchi uliyotoka?” |
610 | GEN 24:18 | Yule msichana akasema, “Kunywa, bwana wangu.” Akashusha kwa haraka mtungi mkononi mwake na akampa, akanywa. |
616 | GEN 24:24 | Yule msichana akamjibu, “Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Milka aliyemzalia Nahori.” |
618 | GEN 24:26 | Yule mtumishi akasujudu na kumwabudu Bwana, |
620 | GEN 24:28 | Yule msichana akakimbia akawaeleza watu wa nyumbani mwa mama yake kuhusu mambo haya. |
657 | GEN 24:65 | na akamuuliza yule mtumishi, “Ni nani mtu yule aliye kule shambani anayekuja kutulaki?” Yule mtumishi akajibu, “Huyu ndiye bwana wangu.” Hivyo Rebeka akachukua shela yake akajifunika. |
661 | GEN 25:2 | Huyu alimzalia Zimrani, Yokshani, Medani, Midiani, Ishbaki na Shua. |
662 | GEN 25:3 | Yokshani alikuwa baba wa Sheba na Dedani, wazao wa Dedani walikuwa Waashuri, Waletushi na Waleumi. |
674 | GEN 25:15 | Hadadi, Tema, Yeturi, Nafishi na Kedema. |
685 | GEN 25:26 | Baadaye, ndugu yake akatoka, mkono wake ukiwa umemshika Esau kisigino; akaitwa jina lake Yakobo. Isaki alikuwa mwenye miaka sitini Rebeka alipowazaa. |
686 | GEN 25:27 | Watoto wakakua, naye Esau akakuwa mwindaji hodari, mtu wa mbugani, wakati Yakobo alikuwa mtu mtulivu, mwenye kukaa nyumbani. |
687 | GEN 25:28 | Isaki, ambaye alikuwa anapendelea zaidi nyama za porini, alimpenda Esau, bali Rebeka alimpenda Yakobo. |
688 | GEN 25:29 | Siku moja Yakobo alipika mchuzi wa dengu, Esau akarudi kutoka porini akiwa na njaa kali. |
689 | GEN 25:30 | Esau akamwambia Yakobo, “Haraka, nipe huo mchuzi mwekundu! Nina njaa kali sana!” (Hii ndiyo sababu pia aliitwa Edomu.) |
690 | GEN 25:31 | Yakobo akamjibu, “Niuzie kwanza haki yako ya mzaliwa wa kwanza.” |
692 | GEN 25:33 | Yakobo akamwambia, “Niapie kwanza.” Hivyo Esau akamwapia, akamuuzia Yakobo haki yake ya kuzaliwa. |
693 | GEN 25:34 | Ndipo Yakobo akampa Esau mkate na ule mchuzi wa dengu. Akala na kunywa, kisha akainuka akaenda zake. Kwa hiyo Esau alidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza. |
704 | GEN 26:11 | Hivyo Abimeleki akatoa amri kwa watu wote, akisema, “Yeyote atakayemnyanyasa mtu huyu au mkewe hakika atauawa.” |
727 | GEN 26:34 | Esau alipokuwa na umri wa miaka arobaini, akamwoa Yudithi binti Beeri Mhiti, kisha akamwoa Basemathi binti Eloni Mhiti. |
734 | GEN 27:6 | Rebeka akamwambia Yakobo mwanawe, “Tazama, nimemsikia baba yako akimwambia ndugu yako Esau, |
739 | GEN 27:11 | Yakobo akamwambia Rebeka mama yake, “Lakini ndugu yangu Esau ana nywele mwilini, mimi nina ngozi nyororo. |
743 | GEN 27:15 | Kisha Rebeka akachukua nguo nzuri za Esau mwanawe wa kwanza, alizokuwa nazo nyumbani, akamvika Yakobo mwanawe mdogo. |
745 | GEN 27:17 | Hatimaye akampa Yakobo hicho chakula kitamu pamoja na mkate aliouoka. |
747 | GEN 27:19 | Yakobo akamwambia baba yake, “Mimi ni Esau mzaliwa wako wa kwanza. Nimefanya kama ulivyoniambia. Tafadhali uketi, ule sehemu ya mawindo yangu ili uweze kunibariki.” |
749 | GEN 27:21 | Kisha Isaki akamwambia Yakobo, “Mwanangu tafadhali sogea karibu nami ili nikupapase, nione kama hakika ndiwe Esau mwanangu, au la.” |
750 | GEN 27:22 | Yakobo akasogea karibu na baba yake Isaki, ambaye alimpapasa na kusema, “Sauti ni ya Yakobo, bali mikono ni ya Esau.” |
753 | GEN 27:25 | Kisha akasema, “Mwanangu, niletee sehemu ya mawindo yako nile, ili nipate kukubariki.” Yakobo akamletea naye akala, akamletea na divai akanywa. |
758 | GEN 27:30 | Baada ya Isaki kumaliza kumbariki na baada tu ya Yakobo kuondoka kwa baba yake, ndugu yake Esau akaingia kutoka mawindoni. |
764 | GEN 27:36 | Esau akasema, “Si ndiyo sababu anaitwa Yakobo? Amenidanganya mara hizi mbili: Alichukua haki yangu ya kuzaliwa na sasa amechukua baraka yangu!” Kisha akauliza, “Hukubakiza hata baraka moja kwa ajili yangu?” |
769 | GEN 27:41 | Esau akawa na kinyongo dhidi ya Yakobo kwa ajili ya baraka ambazo baba yake alikuwa amembariki. Akasema moyoni mwake, “Siku za kuomboleza kwa ajili ya baba yangu zimekaribia, ndipo nitamuua ndugu yangu Yakobo.” |
770 | GEN 27:42 | Rebeka alipokwisha kuambiwa yale aliyoyasema Esau mwanawe mkubwa, alimwita Yakobo mwanawe mdogo, akamwambia, “Ndugu yako Esau anajifariji kwa wazo la kukuua. |
774 | GEN 27:46 | Kisha Rebeka akamwambia Isaki, “Nimechukia kuishi kwa sababu ya hawa wanawake wa Kihiti. Ikiwa Yakobo ataoa mke miongoni mwa wanawake wa nchi hii, wanawake wa Kihiti kama hawa, sitakuwa na faida kuendelea kuishi.” |
775 | GEN 28:1 | Basi Isaki akamwita Yakobo, akambariki na akamwamuru, akisema, “Usioe mwanamke wa Kikanaani. |
779 | GEN 28:5 | Kisha Isaki akamuaga Yakobo, naye akaenda Padan-Aramu, kwa Labani mwana wa Bethueli Mwaramu, ndugu wa Rebeka, aliyekuwa mama wa Yakobo na Esau. |
780 | GEN 28:6 | Sasa Esau akajua kuwa Isaki amembariki Yakobo na kumtuma kwenda Padan-Aramu ili achukue mke huko na kwamba alipombariki alimwamuru akisema, “Usioe mke katika binti za Wakanaani,” |
781 | GEN 28:7 | tena kwamba Yakobo amewatii baba yake na mama yake naye amekwenda Padan-Aramu. |
784 | GEN 28:10 | Yakobo akatoka Beer-Sheba kwenda Harani. |
790 | GEN 28:16 | Yakobo alipoamka kutoka usingizini, akawaza, “Hakika Bwana yuko mahali hapa, wala mimi sikujua.” |
792 | GEN 28:18 | Asubuhi yake na mapema, Yakobo akalichukua lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo na kumimina mafuta juu yake. |
794 | GEN 28:20 | Kisha Yakobo akaweka nadhiri, akisema, “Kama Mungu akiwa pamoja nami na kunilinda katika safari niendayo, akinipa chakula nile na nguo nivae |
797 | GEN 29:1 | Kisha Yakobo akaendelea na safari yake na akafika kwenye nchi za mataifa ya mashariki. |
800 | GEN 29:4 | Yakobo aliwauliza wachungaji, “Ndugu zangu, ninyi mmetoka wapi?” Wakamjibu, “Tumetoka Harani.” |
802 | GEN 29:6 | Kisha Yakobo akawauliza, “Je, yeye ni mzima?” Wakasema, “Ndiyo, ni mzima, na hapa yuaja Raheli binti yake akiwa na kondoo.” |
806 | GEN 29:10 | Yakobo alipomwona Raheli binti Labani, ndugu wa mama yake, pamoja na kondoo wa Labani, alikwenda na kulivingirisha jiwe kutoka mdomoni mwa kisima na kuwanywesha kondoo wa mjomba wake. |
807 | GEN 29:11 | Kisha Yakobo akambusu Raheli na akaanza kulia kwa sauti. |
808 | GEN 29:12 | Yakobo alikuwa amemwambia Raheli kuwa yeye alikuwa jamaa ya baba yake, na kwamba ni mwana wa Rebeka. Basi Raheli alikimbia na kumweleza baba yake. |
809 | GEN 29:13 | Mara Labani aliposikia habari kuhusu Yakobo, mwana wa ndugu yake, aliharakisha kwenda kumlaki. Akamkumbatia na kumbusu, halafu akamleta nyumbani kwake, kisha Yakobo akamwambia mambo yote. |
810 | GEN 29:14 | Ndipo Labani akamwambia, “Wewe ni nyama yangu na damu yangu mwenyewe.” Baada ya Yakobo kukaa kwa Labani mwezi mzima, |
814 | GEN 29:18 | Yakobo akampenda Raheli, akamwambia Labani, “Nitakutumikia kwa miaka saba kwa ajili ya kumpata Raheli binti yako mdogo.” |
816 | GEN 29:20 | Kwa hiyo Yakobo akatumika miaka saba ili kumpata Raheli, lakini ilionekana kwake kama siku chache tu kwa sababu ya upendo wake kwa Raheli. |
817 | GEN 29:21 | Ndipo Yakobo akamwambia Labani, “Nipe mke wangu. Muda wangu umekamilika, nami nataka nikutane naye kimwili.” |
819 | GEN 29:23 | Lakini ilipofika jioni, akamchukua Lea binti yake akampa Yakobo, naye Yakobo akakutana naye kimwili. |
821 | GEN 29:25 | Kesho yake asubuhi, Yakobo akagundua kuwa amepewa Lea! Basi Yakobo akamwambia Labani, “Ni jambo gani hili ulilonitendea? Nilikutumikia kwa ajili ya Raheli, sivyo? Kwa nini umenidanganya?” |
824 | GEN 29:28 | Naye Yakobo akafanya hivyo. Akamaliza juma na Lea, kisha Labani akampa Raheli binti yake kuwa mke wake. |
826 | GEN 29:30 | Pia Yakobo akakutana na Raheli kimwili, naye akampenda Raheli zaidi kuliko Lea. Yakobo akamtumikia Labani kwa miaka mingine saba. |
831 | GEN 29:35 | Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Wakati huu nitamsifu Bwana.” Kwa hiyo akamwita Yuda. Kisha akaacha kuzaa watoto. |
832 | GEN 30:1 | Raheli alipoona hamzalii Yakobo watoto, akamwonea ndugu yake wivu. Hivyo akamwambia Yakobo, “Nipe watoto, la sivyo nitakufa!” |
833 | GEN 30:2 | Yakobo akamkasirikia, akamwambia, “Je, mimi ni badala ya Mungu, ambaye amekuzuia usizae watoto?” |
835 | GEN 30:4 | Hivyo Raheli akampa Yakobo Bilha awe mke wake. Yakobo akakutana naye kimwili, |
836 | GEN 30:5 | Bilha akapata mimba, naye akamzalia Yakobo mwana. |
838 | GEN 30:7 | Bilha mtumishi wa kike wa Raheli akapata mimba tena, akamzalia Yakobo mwana wa pili. |
840 | GEN 30:9 | Lea alipoona kuwa amekoma kuzaa watoto, alimchukua mtumishi wake wa kike Zilpa, naye akampa Yakobo awe mke wake. |
841 | GEN 30:10 | Mtumishi wa Lea yaani Zilpa, akamzalia Yakobo mwana. |
843 | GEN 30:12 | Mtumishi wa kike wa Lea akamzalia Yakobo mwana wa pili. |
846 | GEN 30:15 | Lakini Lea akamwambia, “Haikukutosha kumtwaa mume wangu? Je, utachukua na tunguja za mwanangu pia?” Raheli akasema, “Vema sana! Yakobo atakutana nawe kimwili leo usiku, kwa malipo ya tunguja za mwanao.” |
847 | GEN 30:16 | Kwa hiyo Yakobo alipokuja kutoka shambani jioni ile, Lea akaenda kumlaki, akamwambia, “Lazima ukutane nami kimwili. Nimekukodisha kwa tunguja za mwanangu.” Kwa hiyo akakutana naye kimwili usiku ule. |
848 | GEN 30:17 | Mungu akamsikiliza Lea, naye akapata mimba akamzalia Yakobo mwana wa tano. |