11 | GEN 1:11 | Kisha Mungu akasema, “Ardhi na itoe mimea: miche itoayo mbegu, miti juu ya nchi itoayo matunda yenye mbegu ndani yake, kila mmea kulingana na aina zake mbalimbali.” Ikawa hivyo. |
12 | GEN 1:12 | Ardhi ikachipua mimea: Mimea itoayo mbegu kulingana na aina zake, na miti itoayo matunda yenye mbegu kulingana na aina zake. Mungu akaona ya kuwa hili ni jema. |
16 | GEN 1:16 | Mungu akafanya mianga miwili mikubwa: mwanga mkubwa utawale mchana, na mwanga mdogo utawale usiku. Pia Mungu akafanya nyota. |
24 | GEN 1:24 | Mungu akasema, “Ardhi na itoe viumbe hai kulingana na aina zake: wanyama wa kufugwa, viumbe vitambaavyo ardhini na wanyama pori, kila mnyama kulingana na aina yake.” Ikawa hivyo. |
30 | GEN 1:30 | Nao wanyama wote wa dunia, ndege wote wa angani, na viumbe vyote viendavyo juu ya ardhi: yaani kila kiumbe chenye pumzi ya uhai, ninawapa kila mche wa kijani kuwa chakula.” Ikawa hivyo. |
37 | GEN 2:6 | lakini umande ulitokeza kutoka ardhini na kunyesha uso wote wa nchi: |
148 | GEN 6:10 | Noa alikuwa na wana watatu: Shemu, Hamu na Yafethi. |
153 | GEN 6:15 | Hivi ndivyo utakavyoitengeneza: Safina iwe na urefu wa dhiraa 300, upana wake dhiraa hamsini na kimo chake dhiraa thelathini. |
181 | GEN 7:21 | Kila kiumbe hai kitambaacho juu ya nchi kikaangamia: Ndege, wanyama wa kufugwa, wanyama pori, viumbe vyote juu ya nchi na wanadamu wote. |
201 | GEN 8:17 | Utoe nje kila aina ya kiumbe hai aliye pamoja nawe: Ndege, wanyama na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi, ili wakazae, na kuongezeka na kuijaza tena dunia.” |
214 | GEN 9:8 | Ndipo Mungu akamwambia Noa na wanawe pamoja naye: |
216 | GEN 9:10 | pia na kila kiumbe hai kilichokuwa pamoja nanyi: Ndege, wanyama wa kufugwa na wanyama wote wa porini, wale wote waliotoka katika safina pamoja nanyi, kila kiumbe hai duniani. |
217 | GEN 9:11 | Ninaweka Agano nanyi: Kamwe uhai hautafutwa tena kwa gharika, kamwe haitakuwepo tena gharika ya kuangamiza dunia.” |
218 | GEN 9:12 | Mungu akasema, “Hii ni ishara ya Agano ninalofanya kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, Agano kwa vizazi vyote vijavyo: |
224 | GEN 9:18 | Wana wa Noa waliotoka ndani ya safina ni: Shemu, Hamu na Yafethi. (Hamu ndiye alikuwa baba wa Kanaani.) |
236 | GEN 10:1 | Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika. |
237 | GEN 10:2 | Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi. |
238 | GEN 10:3 | Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma. |
239 | GEN 10:4 | Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu. |
241 | GEN 10:6 | Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani. |
242 | GEN 10:7 | Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani. |
248 | GEN 10:13 | Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi, |
250 | GEN 10:15 | Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi, |
257 | GEN 10:22 | Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu. |
258 | GEN 10:23 | Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki. |
260 | GEN 10:25 | Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani. |
261 | GEN 10:26 | Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera, |
330 | GEN 13:11 | Hivyo Loti akajichagulia bonde lote la Yordani, akaelekea upande wa mashariki. Watu hao wawili wakatengana: |
362 | GEN 15:1 | Baada ya jambo hili, neno la Bwana likamjia Abramu katika maono: “Usiogope, Abramu. Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana.” |
365 | GEN 15:4 | Ndipo neno la Bwana lilipomjia: “Mtu huyu hatakuwa mrithi wako, bali mwana atakayetoka katika viuno vyako mwenyewe ndiye atakayekuwa mrithi wako.” |
393 | GEN 16:11 | Pia malaika wa Bwana akamwambia: “Wewe sasa una mimba nawe utamzaa mwana. Utamwita jina lake Ishmaeli, kwa sababu Bwana amesikia juu ya huzuni yako. |
395 | GEN 16:13 | Hagari akampa Bwana aliyezungumza naye jina hili: “Wewe ndiwe Mungu unionaye mimi,” kwa maana alisema, “Sasa nimemwona yeye anayeniona mimi.” |
402 | GEN 17:4 | “Kwa upande wangu, hili ndilo Agano langu na wewe: Wewe utakuwa baba wa mataifa mengi. |
408 | GEN 17:10 | Hili ni Agano langu na wewe pamoja na wazao wako baada yako, Agano mtakalolishika: Kila mwanaume miongoni mwenu atatahiriwa. |
418 | GEN 17:20 | Kwa upande wa Ishmaeli, nimekusikia: hakika nitambariki, nitamfanya awe na uzao mwingi na nitaongeza sana idadi yake. Atakuwa baba wa watawala kumi na wawili, nami nitamfanya awe taifa kubwa. |
448 | GEN 18:23 | Ndipo Abrahamu akamsogelea akasema: “Je, utawaangamiza wenye haki na waovu? |
452 | GEN 18:27 | Kisha Abrahamu akasema tena: “Sasa kwa kuwa nimekuwa na ujasiri wa kuzungumza na Bwana, ingawa mimi si kitu bali ni mavumbi na majivu; |
509 | GEN 20:13 | Wakati Bwana aliponifanya nisafiri mbali na nyumbani mwa baba yangu, nilimwambia, ‘Hivi ndivyo utakavyoonyesha pendo lako kwangu: Kila mahali tutakapokwenda, kuhusu mimi sema, “Huyu ni kaka yangu.” ’ ” |
568 | GEN 22:20 | Baada ya muda, Abrahamu akaambiwa, “Milka pia amepata watoto, amemzalia ndugu yako Nahori wana: |
572 | GEN 22:24 | Suria wake Nahori aliyeitwa Reuma pia alikuwa na wana: Teba, Gahamu, Tahashi na Maaka. |
588 | GEN 23:16 | Abrahamu akakubali masharti ya Efroni, akampimia ile fedha aliyotaja masikioni mwa Wahiti: Shekeli 400 za fedha kulingana na viwango vya uzito vilivyokuwa vikitumika wakati huo na wafanyabiashara. |
672 | GEN 25:13 | Haya ndiyo majina ya wana wa Ishmaeli, yaliyoorodheshwa kulingana na jinsi walivyozaliwa: Mzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli ni Nebayothi, akafuatia Kedari, Adbeeli, Mibsamu, |
736 | GEN 27:8 | Sasa, mwanangu, nisikilize kwa makini na ufanye yale ninayokuambia: |
756 | GEN 27:28 | Mungu na akupe umande kutoka mbinguni na utajiri wa duniani: wingi wa nafaka na divai mpya. |
764 | GEN 27:36 | Esau akasema, “Si ndiyo sababu anaitwa Yakobo? Amenidanganya mara hizi mbili: Alichukua haki yangu ya kuzaliwa na sasa amechukua baraka yangu!” Kisha akauliza, “Hukubakiza hata baraka moja kwa ajili yangu?” |
771 | GEN 27:43 | Sasa basi, mwanangu, fanya nisemalo: Kimbilia haraka kwa Labani ndugu yangu kule Harani. |
914 | GEN 31:40 | Hii ndiyo iliyokuwa hali yangu: Niliumia kwa joto la mchana na baridi usiku, pia usingizi ulinipa. |
933 | GEN 32:5 | Akawaagiza akisema: “Hili ndilo mtakalomwambia bwana wangu Esau: ‘Mtumishi wako Yakobo anasema, nimekuwa nikiishi pamoja na Labani na nimekuwako huko mpaka sasa. |
942 | GEN 32:14 | Akalala pale usiku ule, miongoni mwa vitu alivyokuwa navyo, akachagua zawadi kwa ajili ya Esau ndugu yake: |
1034 | GEN 35:22 | Wakati Israeli alipokuwa akiishi katika nchi ile, Reubeni mwanawe alikutana kimwili na suria wa baba yake aitwaye Bilha, naye Israeli akasikia jambo hili. Yakobo alikuwa na wana kumi na wawili: |
1035 | GEN 35:23 | Wana wa Lea walikuwa: Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari na Zabuloni. |
1036 | GEN 35:24 | Wana wa Raheli walikuwa: Yosefu na Benyamini. |
1037 | GEN 35:25 | Wana waliozaliwa na Bilha mtumishi wa kike wa Raheli walikuwa: Dani na Naftali. |
1038 | GEN 35:26 | Wana waliozaliwa na Zilpa mtumishi wa kike wa Lea walikuwa: Gadi na Asheri. Hawa walikuwa wana wa Yakobo, waliozaliwa kwake akiwa Padan-Aramu. |
1043 | GEN 36:2 | Esau akaoa wake kutoka miongoni mwa wanawake wa Kanaani: Ada binti wa Eloni Mhiti, Oholibama binti wa Ana, mjukuu wa kike wa Sibeoni Mhivi, |
1051 | GEN 36:10 | Haya ndiyo majina ya wana wa Esau: Elifazi, mwana wa Esau ambaye mkewe Ada alimzalia; na Reueli, mwana wa Esau ambaye mkewe Basemathi alimzalia. |
1052 | GEN 36:11 | Wana wa Elifazi ni: Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi. |
1054 | GEN 36:13 | Wana wa Reueli ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Basemathi mkewe Esau. |
1055 | GEN 36:14 | Wana wa Oholibama binti Ana, mkewe Esau, aliyekuwa mjukuu wa Sibeoni, aliomzalia Esau ni: Yeushi, Yalamu na Kora. |
1056 | GEN 36:15 | Hawa ndio waliokuwa wakuu miongoni mwa wazao wa Esau: Wakuu wa wana wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau ni: Temani, Omari, Sefo, Kenazi, |
1058 | GEN 36:17 | Wakuu wa wana wa Reueli, mwana wa Esau ni: Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa Reueli huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Basemathi mkewe Esau. |
1059 | GEN 36:18 | Wakuu wa wana wa Esau ambao mkewe Oholibama alimzalia ni: Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa mke wa Esau, Oholibama binti Ana. |
1061 | GEN 36:20 | Hawa ndio walikuwa wana wa Seiri, Mhori, waliokuwa wakiishi katika nchi ile: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana, |
1063 | GEN 36:22 | Wana wa Lotani walikuwa: Hori na Homamu. Timna alikuwa dada yake Lotani. |
1064 | GEN 36:23 | Wana wa Shobali walikuwa: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo na Onamu. |
1065 | GEN 36:24 | Wana wa Sibeoni walikuwa: Aiya na Ana. Huyu Ana ndiye aligundua chemchemi ya maji moto jangwani alipokuwa akichunga punda za Sibeoni baba yake. |
1066 | GEN 36:25 | Watoto wa Ana walikuwa: Dishoni na Oholibama binti wa Ana. |
1067 | GEN 36:26 | Wana wa Dishoni walikuwa: Hemdani, Eshbani, Ithrani na Kerani. |
1068 | GEN 36:27 | Wana wa Eseri walikuwa: Bilhani, Zaavani na Akani. |
1069 | GEN 36:28 | Wana wa Dishani walikuwa: Usi na Arani. |
1070 | GEN 36:29 | Hawa ndio waliokuwa wakuu wa Wahori: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana, |
1072 | GEN 36:31 | Wafuatao ni wafalme waliotawala Edomu kabla ya mfalme yeyote wa Israeli kutawala: |
1081 | GEN 36:40 | Hawa ndio wakuu waliotokana na Esau, kwa majina, kufuatana na koo zao na nchi zao: Timna, Alva, Yethethi, |
1090 | GEN 37:6 | Akawaambia, “Sikilizeni ndoto niliyoota: |
1167 | GEN 39:17 | Ndipo akamweleza kisa hiki, akisema: “Yule mtumwa wa Kiebrania uliyetuletea alinijia ili kunidhihaki. |
1185 | GEN 40:12 | Yosefu akamwambia, “Hii ndiyo maana yake: Matawi matatu ni siku tatu. |
1189 | GEN 40:16 | Yule mwokaji mkuu alipoona kuwa Yosefu amefasiri ikiwa na maana nzuri, akamwambia Yosefu, “Mimi pia niliota ndoto: Kichwani mwangu kulikuwepo vikapu vitatu vya mikate. |
1191 | GEN 40:18 | Yosefu akamwambia, “Hii ndiyo maana yake: Vikapu vitatu ni siku tatu. |
1193 | GEN 40:20 | Mnamo siku ya tatu, ilikuwa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Farao, naye akawaandalia maafisa wake wote karamu. Akawatoa gerezani mnyweshaji mkuu na mwokaji mkuu, akawaweka mbele ya maafisa wake: |
1197 | GEN 41:1 | Baada ya miaka miwili kamili kupita, Farao aliota ndoto: Tazama alikuwa amesimama kando ya Mto Naili, |
1201 | GEN 41:5 | Farao akaingia usingizini tena akaota ndoto ya pili: Akaona masuke saba ya nafaka, yenye afya na mazuri, yanakua katika bua moja. |
1209 | GEN 41:13 | Nayo mambo yakawa sawa kabisa na jinsi alivyotufasiria ndoto zetu: Mimi nilirudishwa kazini mwangu na huyo mtu mwingine akaangikwa.” |
1224 | GEN 41:28 | “Ni kama vile nilivyomwambia Farao: Mungu amemwonyesha Farao jambo analokusudia kufanya karibuni. |
1267 | GEN 42:14 | Yosefu akawaambia, “Ni sawa kabisa kama nilivyowaambia: Ninyi ni wapelelezi! |
1268 | GEN 42:15 | Na hivi ndivyo mtakavyojaribiwa: Hakika kama Farao aishivyo, hamtaondoka mahali hapa mpaka ndugu yenu mdogo aje hapa. |
1271 | GEN 42:18 | Siku ya tatu Yosefu akawaambia, “Fanyeni hili nanyi mtaishi, kwa maana namwogopa Mungu: |
1286 | GEN 42:33 | “Ndipo huyo mtu aliye bwana katika nchi hiyo alipotuambia, ‘Hivi ndivyo nitafahamu kuwa ninyi ni watu waaminifu: Mwacheni mmoja wa ndugu zenu pamoja nami hapa, kisha nendeni mpeleke chakula kwa ajili ya jamaa yenu inayoteseka kwa njaa. |
1302 | GEN 43:11 | Basi baba yao Israeli akawaambia, “Kama ni lazima iwe hivyo, basi fanyeni hivi: Wekeni baadhi ya mazao bora ya nchi katika mifuko yenu na mpelekeeni yule mtu kama zawadi, zeri kidogo, asali kidogo, vikolezo, manemane, kungu na lozi. |
1326 | GEN 44:1 | Kisha Yosefu akampa yule msimamizi wa nyumbani mwake maagizo haya: “Jaza magunia ya watu hawa kiasi cha chakula ambacho wanaweza kuchukua, na uweke fedha ya kila mtu kwenye mdomo wa gunia lake. |
1343 | GEN 44:18 | Ndipo Yuda akamwendea na kumwambia: “Tafadhali bwana wangu, mruhusu mtumishi wako aseme neno kwa bwana wangu. Usimkasirikie mtumishi wako, ingawa wewe ni sawa na Farao mwenyewe. |
1368 | GEN 45:9 | Sasa rudini haraka kwa baba yangu na mwambieni, ‘Hili ndilo mwanao Yosefu asemalo: Mungu amenifanya mimi kuwa bwana wa Misri yote. Shuka uje kwangu, wala usikawie. |
1376 | GEN 45:17 | Farao akamwambia Yosefu, “Waambie ndugu zako, ‘Fanyeni hivi: Pakieni wanyama wenu mrudi mpaka nchi ya Kanaani, |
1378 | GEN 45:19 | “Mnaagizwa pia kuwaambia, ‘Fanyeni hivi: Chukueni magari ya kukokotwa kutoka Misri, kwa ajili ya watoto wenu na wake zenu, mkamchukue baba yenu mje. |
1382 | GEN 45:23 | Hivi ndivyo vitu alivyotuma kwa baba yake: punda kumi waliochukua vitu vizuri vya Misri, punda wake kumi waliobeba nafaka, mikate na mahitaji mengine ya safari. |
1395 | GEN 46:8 | Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli (Yakobo na wazao wake), waliokwenda Misri: Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo. |
1396 | GEN 46:9 | Wana wa Reubeni ni: Hanoki, Palu, Hesroni na Karmi. |
1397 | GEN 46:10 | Wana wa Simeoni ni: Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli mwana wa mwanamke Mkanaani. |
1398 | GEN 46:11 | Wana wa Lawi ni: Gershoni, Kohathi na Merari. |
1399 | GEN 46:12 | Wana wa Yuda ni: Eri, Onani, Shela, Peresi na Zera (lakini Eri na Onani walifariki katika nchi ya Kanaani). Wana wa Peresi ni: Hesroni na Hamuli. |
1400 | GEN 46:13 | Wana wa Isakari ni: Tola, Puva, Yashubu na Shimroni. |