Wildebeest analysis examples for:   swh-swhulb   N    February 11, 2023 at 19:39    Script wb_pprint_html.py   by Ulf Hermjakob

2  GEN 1:2  Nayo nchi haikuwa na umbo na ilikuwa tupu. Giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji. Roho wa Mungu alikuwa akielea juu ya uso wa maji.
12  GEN 1:12  Nchi ikatoa mimea, miche itoayo mbegu ya aina yake, na miti itoayo tunda ambalo mbegu yake imo ndani yake, kwa aina yake. Mungu akaona kuwa ni vyema.
14  GEN 1:14  Mungu akasema, “kuwe na mianga katika anga kutenganisha mchana na usiku. Na ziwe kama ishara, kwa majira, kwa siku na miaka.
22  GEN 1:22  Mungu akavibariki, akisema, “zaeni na muongezeke, na mjae majini katika bahari. Ndege waongezeke juu nchi.”
41  GEN 2:10  Mto ukatoka nje ya Edeni kuitia maji bustani. Na kutoka pale ukagawanyika na kuwa mito minne.
49  GEN 2:18  Kisha Yahwe Mungu akasema, “siyo jambo jema kwamba mtu huyu lazima awe pekeyake. Nitamfanyia msaidizi anaye mfaa.”
60  GEN 3:4  Nyoka akamwambia mwanamke, “hakika hamtakufa.
62  GEN 3:6  Na mwanamke alipoona kuwa mti ni mzuri kwa chakula, na kuwa unapendeza macho, na kwamba mti ulitamanika kwa kumfanya mtu awe mwerevu, alichukua sehemu ya tunda na akala. Na sehemu yake pia akampatia mumewe aliyekuwa naye, naye akala.
67  GEN 3:11  Mungu akasema,Ni nani alikwambia kuwa ulikuwa uchi? Je umekula kutoka mti ambao nilikuagiza usile matunda yake?”
69  GEN 3:13  Yahwe Mungu akamwambia mwanamke, Nini hiki ulichofanya?” mwanamke akasema,nyoka alinidanganya, na nikala.”
71  GEN 3:15  Nitaweka uadui kati yako na mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake. Atakujeruhi kichwa chako na utamjeruhi kisigino chake.”
88  GEN 4:8  Kaini akamwambia Habili ndugu yake. Hata wakati walipokuwa shambani, Kaini aliinuka dhidi ya Habili ndugu yake na akamuua. (Katika tafsiri za kale zinasema, Kaini alimwambia Habili ndugu yake, “ twende mashambani.” Na wakati walipokuwa shambani, Kaini alimuinukia Habili ndugu yake na kumuua).
89  GEN 4:9  Kisha Yahwe akamuuliza Kaini, Ndugu yako Habili yuko wapi?” Akasema, “sijui. Je mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?”
91  GEN 4:11  Na sasa umelaaniwa wewe kutoka ardhi ambayo imefungua kinywa chake kupokea damu ya ndugu yako kutoka mikononi mwako.
94  GEN 4:14  Kwa hakika umenifukuza siku hii ya leo kutoka kwenye ardhi hii, na sitaonekana mbele ya uso wako. Nitakuwa mkimbizi na mtu nisiye na makao katika dunia, na yeyote atakaye niona ataniua.”
96  GEN 4:16  Kwa hiyo Kaini akatoka mbele ya uwepo wa Yahwe na akaishi katika nchi ya Nodi, mashariki mwa Edeni.
101  GEN 4:21  Ndugu yake aliitwa Yubali. Huyu alikuwa baba yao na wale wapigao kinubi na filimbi.
102  GEN 4:22  Sila naye akamzaa Tubal Kaini, mfua vyombo vya shaba na chuma. Dada yake na Tubal Kaini alikuwa Naama.
135  GEN 5:29  Akamuita jina lake Nuhu, akisema, “Huyu ndiye atatupatia pumziko kutoka katika kazi yetu na kutoka katika kazi ya taabu ya mikono yetu, ambayo lazima tuifanye kwa sababu ya ardhi ambayo Yahwe ameilaani.”
136  GEN 5:30  Lameki aliishi miaka 595 baada ya kumzaa baba wa Nuhu. Akazaa wanawengi wa ume na wake.
138  GEN 5:32  Baada ya Nuhu kuishi miaka miatano, akamzaa Shemu, Hamu, na Yafethi.
145  GEN 6:7  Kwa hiyo Yahwe akasema,Nitamfutilia mbali mwanadamu ambaye nimemuumba katika uso wa nchi; mwanadamu na wanyama wakubwa, na vitambaavyo na ndege wa angani, kwa kuwa nimehuzunika kuwa nimeviumba.”
146  GEN 6:8  Lakini Nuhu akapata neema ya upendeleo machoni pa Yahwe.
147  GEN 6:9  Kulikuwa na matukio kumuhusu Nuhu. Nuhu alikuwa mtu mwenye haki, na asiye na lawama miongoni mwa watu wa kipindi chake. Nuhu alitembea na Mungu.
148  GEN 6:10  Nuhu akafanyika baba wa wana watatu wa kiume: Shem, Ham na Yafeti.
149  GEN 6:11  Nchi iliharibika mbele za Mungu, na ikajaa ghasia.
151  GEN 6:13  Mungu akamwambia Nuhu, Nimeona kuwa sasa niwakati wa mwisho kwa wote wenye mwili, kwa kuwa inchi imejaa ghasia kutokana na wao. Hakika, nitawaharibu wao pamoja na nchi.
160  GEN 6:22  Kwa hiyo Nuhu akafanya hivi. kulingana na yote ambayo Mungu alimuagiza, ndivyo alifanya.
161  GEN 7:1  Yahwe akamwambia Nuhu, Njoo, wewe na nyumba yako wote, katika safina, kwa kuwa nimeona kuwa wewe ni mwenye haki mbele yangu katika kizazi hiki.
162  GEN 7:2  Kwa kila mnyama aliye safi utakuja nao saba wa kiume na saba wa kike. Na kwa wanyama wasio safi, lete wawili wawili, wakiume na wakike.
164  GEN 7:4  Kwa kuwa ndani ya siku saba nitasababisha mvua kunyesha juu ya nchi muda wa siku arobaini mchana na usiku. Nitaharibu kila kiumbe hai nilichokiumba juu ya uso wa ardhi.”
165  GEN 7:5  Nuhu alifanya yote ambayo Yahwe alimuagiza.
166  GEN 7:6  Nuhu alikuwa na umri wa miaka mia sita wakati gharika ilipokuja juu ya nchi.
167  GEN 7:7  Nuhu, watoto wake wa kiume, mke wake, na wake za watoto wake waliingia katika safina pamoja kwa sababu ya maji ya gharika.
169  GEN 7:9  wawili wawili mume na mke wakaja kwa Nuhu na wakaingia katika safina, kama vile Mungu alivyokuwa amemwagiza Nuhu.
171  GEN 7:11  Katika mwaka wa mia sita wa maisha yake Nuhu, katika mwezi wa pili, katika siku ya kumi na saba ya mwezi, katika siku iyo hiyo, chemchemi zote za vilindi vikuu zilipasuka na kufunguka, na madirisha ya mbinguni yakafunguka.
173  GEN 7:13  Katika siku iyo hiyo Nuhu pamoja na watoto wake, Shem, Ham, na Yafethi na mke wa Nuhu, na wale wake watatu wa wana wa Nuhu pamoja waliingia katika safina.
175  GEN 7:15  Viwili viwili katika kila chenye mwili ambacho kilikuwa na pumzi ya uhai kilikuja kwa Nuhu na kuingia katika safina.
183  GEN 7:23  Hivyo kila kilichokuwa hai ambacho kilikuwa juu ya uso wa mchi kilifutwa, kuanzia watu mpaka wanyama wakubwa, mpaka vitambaavyo, na mpaka ndege wa angani. Vyote viliangamizwa kutoka kwenye nchi. Nuhu tu pamoja na wale waliokuwa naye kwenye safina ndio walisalia.
185  GEN 8:1  Mungu akamtazama Nuhu, wanyama wote wa mwitu, na wanyama wote wa kufugwa ambao walikuwa pamoja naye kwenye safina. Mungu akafanya upepo uvume juu ya nchi, na maji yakaanza kuzama chini.
190  GEN 8:6  Ikatokea kwamba baada ya siku arobaini Nuhu alifungua dirisha la safina ambayo aliitengeneza.
195  GEN 8:11  Njiwa akarudi kwake jioni. Tazama! katika mdomo wake kulikuwa na jani bichi la mzeituni lililochumwa. Kwa hiyo Nuhu akatambua kuwa maji yamekwisha zama chini ya nchi.
196  GEN 8:12  Akasubiri siku saba zingine na akamtuma njiwa tena. Njiwa hakurudi kwake tena.
197  GEN 8:13  Ikawa kwamba katika mwaka wa mia sita na moja, katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, maji yalikuwa yamekauka katika nchi. Nuhu akaondoa kifuniko cha safina, akatazama nje, na akaona kwamba, Tazama, uso wa nchi ulikuwa umekauka.
199  GEN 8:15  Mungu akamwambia Nuhu,
202  GEN 8:18  Kwa hiyo Nuhu akatoka nje pamoja na watoto wake wa kiume, mke wake, na wake wa wa wanawe pamoja naye.
204  GEN 8:20  Nuhu akajenga madhabahu kwa Yahwe. Akachukua baadhi ya wanyama walio safi na baadhi ya ndege walio safi, na kutoa sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu.
207  GEN 9:1  Kisha Mungu akambariki Nuhu na wanawe, na kuwaambia, “Zaeni, mkaongezeke, na muijaze nchi.
213  GEN 9:7  Na hivyo nanyi zaeni na kuongezeka, sambaeni katika inchi yote na muongezeke juu yake.”
214  GEN 9:8  Kisha Mungu akazungumza na Nuhu na wanae pamoja naye, akisema,
215  GEN 9:9  “Kwa ajili yangu, sikiliza! Ninakwenda kulithibitisha agano langu pamoja nawe na uzao wenu baada yenu,
219  GEN 9:13  Nimeweka upinde wangu wa mvua katika wingu, na itakuwa ndiyo ishara ya agano kati yangu na nchi.
223  GEN 9:17  Kisha Mungu akamwambia Nuhu, “ Hii ni ishara ya agano ambalo nimelithibitisha kati yangu na wenye mwili wote ambao wako juu ya nchi.”
224  GEN 9:18  Wana wa Nuhu ambao walitoka katika safina walikuwa ni Shemu, Hamu, na Yafethi. Na Hamu akamzaa kanaani.
225  GEN 9:19  Watatu hawa walikuwa ndio wana wa Nuhu, na kutokea kwa hawa nchi yote ikajaa watu.
226  GEN 9:20  Nuhu akaanza kuwa mkulima, na akapanda mizabibu.
229  GEN 9:23  Kwa hiyo Shemu na Yafethi wakachukua kanzu wakaitanda juu ya mabega yao, na wakatembea kinyumenyume na wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zikiwa zimegeuka nyuma upande mwingine, kwa hiyo hawakuona uchi wa baba yao.
230  GEN 9:24  Nuhu alipozinduka kutoka katika ulevi wake, alijua ni jambo gani mtoto wake mdogo amemfanyia.
231  GEN 9:25  Hivyo akasema, “Alaaniwe Kanaani. Na awe mtumishi kwa watumishi wa ndugu zake.”
234  GEN 9:28  Baada ya gharika, Nuhu aliishi miaka miatatu na hamsini.
235  GEN 9:29  Siku zote za Nuhu zilikuwa ni miaka mia tisa na hamsini, na kisha alikufa.
236  GEN 10:1  Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya wana wa Nuhu, ambao ni, Shemu, Hamu, na Yafethi. Wana wa kiume walizaliwa kwao baada ya gharika.
238  GEN 10:3  Na wana wa Gomeri walikuwa Ashikenazi, Rifathi na Togama.
243  GEN 10:8  Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikuwa hodari wa kwanza juu ya nchi.
244  GEN 10:9  Alikuwa mwindaji mkuu mbele ya Yahwe. Hii ndiyo sababu hunenwa, “Kama Nimrod mwindaji mkuu mbele za Yahwe.”
246  GEN 10:11  Kutoka katika nchi ile alikwenda Ashuru na akajenga Ninawi, Rehoboth- iri na Kala,
247  GEN 10:12  na Raseni ambao ulikuwa kati ya Ninawi na Kala. Ulikuwa mji mkubwa.
267  GEN 10:32  Hizi zilikuwa koo za wana wa Nuhu, kulingana na vizazi vyao, kwa mataifa yao. Kutokea kwa hawa mataifa yaligawanyika na kwenda juu ya nchi baada ya gharika.
274  GEN 11:7  Njoni, tushuke na tuvuruge lugha yao pale, ili kwamba wasielewane.”
289  GEN 11:22  Wakati Seregu alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Nahori.
290  GEN 11:23  Seregu aliishi miaka mia mbili baada ya kumzaa Nahori. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
291  GEN 11:24  Wakati Nahori alipokuwa ameishi miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
292  GEN 11:25  Nahori aliishi mika 119 baada ya kumzaa Tera. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
293  GEN 11:26  Baada ya Tera kuishi miaka sabini, akamzaa Abram, Nahori, na Haran.
294  GEN 11:27  Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Tera. Tera alimzaa Abram, Nahori, na Harani, na Harani akamzaa Lutu.
296  GEN 11:29  Abram na Nahori wakajitwalia wake. Mke wa Abram aliitwa Sarai na mke wa Nahori aliitwa Milka, binti wa Harani, aliyekuwa baba wa Milka na Iska.
300  GEN 12:1  Kisha Yahwe akamwambia Abram,Nenda utoke katika nchi yako, na toka kwa ndugu zako, na kwa jamaa za baba yako, uende katika nchi nitakayo kuonesha.
301  GEN 12:2  Nitakufanya uwe taifa kubwa, na nitakubariki na kulifanya jinalako kuwa kubwa, na utafanyika baraka.
302  GEN 12:3  Nitawabariki wakubarikio, lakini asiye kuheshimu nita mlaani. Kupitia kwako familia zote za nchi zitabarikiwa.
306  GEN 12:7  Yahwe akamtokea Abram, na kusema,Nitawapa uzao wako nchi hii.” Kwa hiyo Abram akamjengea madhabahu, Yahwe ambaye alimtokea.
308  GEN 12:9  Kisha Abram akaendelea kusafiri, akielekea upande wa Negebu.
317  GEN 12:18  Farao akamwita Abram na kusema,Nini hiki ambacho umenifanyia? Kwa nini hukuniambia kuwa alikuwa mke wako?
320  GEN 13:1  Kwa hiyo Abram akaondoka akatoka Misri na akaenda Negebu, Yeye, mke wake, na vyote alivyokuwa navyo. Lutu pia akaenda pamoja naye.
321  GEN 13:2  Na sasa Abram alikuwa tajiri wa mifugo, fedha na dhahabu.
322  GEN 13:3  Aliendelea na safari yake kutoka Negebu hadi Betheli, mahali ambapo hema yake ilikuwa tangu mwanzo, kati ya Betheli na mji wa Ai.
325  GEN 13:6  Nchi haikuwatosha wote kukaa pamoja karibu kwa sababu mali zao zilikuwa nyingi sana, kiasi kwamba hawakuweza kukaa pamoja.
328  GEN 13:9  Je nchi hii yote haiko mbele yako? Nenda na ujitenge na mi. Ikiwa utakwenda kushoto, mimi nitakwenda kulia. au ikiwa utakwenda kulia, mimi nitakwenda kushoto.”
332  GEN 13:13  Na sasa watu wa Sodoma walikuwa waovu na wenye dhambi nyingi dhidi ya Yahwe.
334  GEN 13:15  Nchi yote hii uionayo, nitakupatia wewe pamoja na uzao wako milele.
335  GEN 13:16  Nitawafanya uzao wako kuwa wengi kama mavumbi ya nchi, kiasi kwamba kama kuna mtu anaweza kuhesabu mavumbi ya nchi, ndipo na uzao wako pia utahesabika.
347  GEN 14:10  Na sasa bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya lami, na wafalme wa Sodoma na Gomora walipokimbia, wakaanguka pale. Wale waliosalia wakakimbilia milimani.
358  GEN 14:21  Mfalme wa Sodama akamwambia Abram,Nipatie watu, na ujichukulie wewe mwenyewe mali.”
359  GEN 14:22  Abram akamwambia mfalme wa Sodoma,Nimeinua juu mkono wangu kwa Yahwe, Mungu aliye juu sana, muumbaji wa mbingu na nchi,
370  GEN 15:9  Kisha akamwambia,Nipatie ndama wa umri wa miaka mitatu, mbuzi mke wa umri wa miaka mitatu, na kondoo mume wa umri wa miaka mitatu, na njiwa na mwana njiwa.”
375  GEN 15:14  Nitahukumu taifa ambalo watalitumikia, na baadye watatoka wakiwa na mali nyingi.
379  GEN 15:18  Siku hiyo Yahwe akafanya agano na Abram, akisema,Ninatoa nchi hii kwa uzao wako, kutoka mto wa Misri hadi kwenye mto mkuu, Frati -