Wildebeest analysis examples for:   swh-swhulb   i    February 11, 2023 at 19:39    Script wb_pprint_html.py   by Ulf Hermjakob

1  GEN 1:1  Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na nchi.
2  GEN 1:2  Nayo nchi haikuwa na umbo na ilikuwa tupu. Giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji. Roho wa Mungu alikuwa akielea juu ya uso wa maji.
3  GEN 1:3  Mungu akasema, “na kuwe nuru,” na kulikuwa na nuru.
4  GEN 1:4  Mungu akaona nuru kuwa ni njema. Akaigawa nuru na giza.
5  GEN 1:5  Mungu akaiita nuru “ mchana” na giza akaliita “usiku.” Ikawa jioni na asubuhi, siku ya kwanza.
6  GEN 1:6  Mungu akasema, “ na kuwe na anga kati ya maji, na ligawe maji na maji.”
7  GEN 1:7  Mungu akafanya anga na kugawanya maji yaliyo kuwa chini ya anga na maji ambayo yalikuwa juu ya anga. Ikawa hivyo.
8  GEN 1:8  Mungu akaita anga “mbingu.” Ikawa jioni na asubuhi siku ya pili.
9  GEN 1:9  Mungu akasema, “maji yaliyo chini ya mbingu yakusanyike pamoja mahali pamoja, na ardhi kavu ionekane.” Ikawa hivyo.
10  GEN 1:10  Mungu aliita ardhi kavu “nchi,” na maji yaliyo kusanyika akayaita “bahari.” Akaona kuwa ni vyema.
11  GEN 1:11  Mungu akasema, nchi ichipushe mimea: miche itoayo mbegu na miti ya matunda itoayo matunda ambayo mbegu yake imo ndani ya tunda, kila kitu kwa namna yake.” Ikawa hivyo.
12  GEN 1:12  Nchi ikatoa mimea, miche itoayo mbegu ya aina yake, na miti itoayo tunda ambalo mbegu yake imo ndani yake, kwa aina yake. Mungu akaona kuwa ni vyema.
13  GEN 1:13  Ikawa jioni na asubuhi, siku ya tatu.
14  GEN 1:14  Mungu akasema, “kuwe na mianga katika anga kutenganisha mchana na usiku. Na ziwe kama ishara, kwa majira, kwa siku na miaka.
15  GEN 1:15  Ziwe mianga katika anga ili kutoa mwanga juu ya nchi.” Ikawa hivyo.
16  GEN 1:16  Mungu akafanya mianga mikuu miwili, mwanga mkuu zaidi kutawala mchana, na mwanga mdogo kutawala usiku. Akafanya nyota pia.